Skip to main content

Posts

Showing posts with the label Mastori

RUDI KWA MAMA

Wino huu uliomwagika umeandikwa Na yatima asiye Na baba wala mama! Mwenye machungu ya kumbukumbu kila atazamapo picha za wazazi wake! Mwenye tamaa yakuzungumza Na mama kumwambia anampenda! Nakushauriana na baba jinsi dunia inavyokwenda. Leo wino wangu umebeba dhamira yakukumbusha urudi kwa Mama. Usiseme hakuna sababu yamsingi yakwenda kumsalimia mama! Ukifanyacho kinakupa riziki, mafanikio na utajiri lakini vitu hivyo ni vichungu siku utakapokuwa huwaoni wazazi wako. Siku watakapokuwa mbali Na upeo wa macho yako! Siku nawewe utakapokuwa yatima. Rudi kwamama! Nenda kamwambie unampenda sana! Kaseme nae yote yakwako naumsikilize yote yakwake. Hakikisha anafarijika kwa uwepo wako! Usitoe hata dakika akahisi upweke! Akahisi umemtenga nakuzipa thamani kazi zako au watu wako wengine ulionao. Kumbuka wao wanakuona wamuhimu, mwenye nguvu Na wathamani! Kwasababu ya juhudi za wazazi wako. Walikesha nawewe ulipokuwa unawasumbua ukilia usiku kucha enzi za uchanga wako. Walihakikisha unanyamaza ha

MAFANIKIO; ukihitaji ufanikiwe fanya haya

Wakati huu ambao kila mtu anapambana nahali yake, ujasiriamali umekua kimbilio la vijana wengi, kama tunavyojua hakuna mtu anaeanzisha kitu kwa lengo la kufeli , japo sio wote hufanikiwa. Leo nawaletea sifa 4 za wajasiriamali waliofanikiwa na pengine ukiziiga, unaweza kuongeza nafasi ya kufanikiwa katika mishe zako. 1. PENDELEA KUAMKA MAPEMA Huwezi fanikisha malengo yako kama wewe ni mtumwa wa usingizi. siku zote pendelea kuamka mapema ili uweze kukamilisha kazi zilizobaki au ngumu ambazo unatakiwa uzikamilishe kwa siku husika maana  akili yako inakuwa bado ina nguvu ya kufanya mambo mengi na kwa ufanisi wakati wa asubuhi. mabilionea wengi duniani ikiwemo Mo Dewji, Bakhlesa, Dangote n.k. wana tabia ya kuamka mapema 2. PANGA SIKU YAKO MAPEMA  Ni vizuri kupangilia siku yako mapema ili kujua uamkapo utaanza na nini. Hii husaidia kazi zako kufanyika kwa mpangilio na kuokoa muda ambao utaruhusu akili yako kufanya kazi na kuvumbua vitu vya nyongeza. Pia itapelekea kuboresha bi

HEBU SOMA HII KWA MAKINI ITAKUSAIDIA SANA NA ITAKUGUSA TU

MAFANIKIO YA MAISHA SIO ELIMU TU, bali UTHUBUTU, KUJIAMINI NA UJASIRI WA MAAMUZI... ✍🏽Ukichunguza katika jamii, utabaini kuwa sehemu kubwa ya matajiri ni wale ambao wana elimu ndogo ama hawakusoma kabisa. 👉🏾Katika miji na maeneo yote; wenye majengo ya maana, wenye makampuni makubwa, wenye utitiri wa malori na mabasi, wenye maduka makubwa wengi wao ni wale wa elimu ya chini kabisa, "darasa la saba” ama wale ambao hawakuingia darasani kabisa... 🙇🏽📚 Wasomi wengi wana maisha ya kawaida yaani yale ya kiwango cha kubadilisha mboga, wakijitahidi sana wanaishia kujenga nyumba za kuishi 🏡 na 🚗 🚙magari mawili ya kutembelea (tena kwa mikopo!) 👉🏾Wapo 🙇🏽📚wasomi wengi tu wanaoishi kimasikini, kwa lugha ya kistaarabu tunasema wana maisha ya kuungaunga. Kiukweli idadi ya wasomi walio matajiri ni ndogo sana.. 👉🏾Lakini Umasikini wa wasomi wengi umeanzia huko shuleni na vyuoni wanakopatia usomi wao. Madarasani kuna mambo mawili wanafundishwa wasomi ambayo ndio yanayow

DKT LOUS SHIKA TAYARI KUTUMIWA MABILION YAKE KUTOKA URUSI

Dkt. Louis Shika ambaye alijizolea umaarufu baada ya kutangaza dau kununua nyumba tatu za mfanyabiashara Said Lugumi kwa shilingi bilioni 3.2 zilizokuwa zikipigwa mnada na kampuni ya Yono lakini akashindwa kulipa asilimia 25 ya fedha hizo, ameanza mchakato wa kurejesha fedha zake zilizopo nje ya nchi. Amesema kuwa leo jumamosi amelipa Dola 100 za Kimarekani sawa na shilingi (220,000) za Kitanzania kwa ajili ya bima ili aweze kutumiwa fedha zake nchini. Dkt. Shika amesema hayo mara baada ya kukutana na waandishi wa habari waliokuwa katika ziara ya Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye alipokuwa ametembelea Shirika la Posta kuzungumza na wafanyakazi, walimkuta Dkt. Shika akiwa katika shirika hilo, na kudai kuwa yupo hapo kwa ajili ya malipo. “Nimelipa dola 100 za bima ili kukamilisha fedha zangu zije na nilipie zile nyumba, hili la bima lilikuwa ni muhimu sana kwangu,”amesema Dkt. Shika Hata hivyo, nyumba moja ilishauzwa kwa mhindi aliyeshika namba mbili

Simulizi ya mapenzi

Nilikua mwajiriwa katika kampuni moja maarufu jijini dare s salaam , katika kuajiriwa kwangu huko nikawa msaidizi maalumu wa bosi wa kampuni ile , basi siku moja moja nilikuwa naenda kujirusha na bosi wangu .   Ukizingatia kwamba sikuwa na mume wala mchumba na kwa kweli huyu bosi ndio alikuwa mtu wa kwanza kufanya nae tendo la ndoa , hivyo nilifurahia mhemko wake na jinsi alivyokuwa ananipenda na kunijali kila kitu nilipata na zaidi . Alifanya yote haya bila kunificha kwamba ana mke na watoto nyumbani kwake kwahiyo wakati mwingine chochote kinaweza kutokea nijiandae kwa shuguli hiyo pevu kama mke wake akishitukia dili hilo . Tulikuwa na uhusiano na huyu bosi kwa miezi 4 hivi mpaka siku moja katika tembea tembea mitaani nikakutana na kijana mmoja mtanashati akanieleza kwamba ananipenda na kunizimia sana yaani ameshanifia Huyu kijana alihangaika kwa mwezi mzima mpaka siku nikaja kumkubalia akawa ndio mpenzii wangu halali sasa , nilimwamini sana nay eye aliniamini sana , miezi 3 t

SIMULIZI YA KWELI YA KUSISIMUA NA KUSIKITISHA YA MTOTO JANETH :

Kengele ya kutoka darasani iligongwa, wanafunzi wa shule ya msingi wakaanza kutoka madarasani huku wakifukuzana wengine wakipiga kelele ilimradi shwangwe tu. Ilikuwa mara yangu ya kwanza kufundisha shule za hatua hiyo. Ilikuwa ni shule ya serikali. Jicho langu liliangukia katika sura ya msichana mdogo, nguo zake chafu. Alikuwa analia. Alikuwa peke yake na hakuwa na yeyote wa kumbembeleza. Mimi kama mwalimu sikutaka kujisogeza karibu naye sana. Kwanza nilikuwa mgeni. Nikaachana naye. Siku iliyofuata tukio kama lile likajirudia. Msichana yuleyule wakati ule uleule wa kutawanyika, alikuwa analia sana. Mwishowe aliondoka huku akiwa analia. “Mbona mwenzenu analia?” nilimuuliza mwanafunzi mmoja. “Huyo ni mama kulialia..” alinijibu huku anacheka. Haikuniingia akilini hata kidogo kuwa yule binti analia bila sababu. Siku ya tatu nikaanza kujiweka karibu naye. Muda wa mapumziko nilimwita nikamnunulia chai, alikuwa ananiogopa na hakutaka kuniangalia machoni. Sikumuuliza lolote juu ya tabia ya

SIMULIZI YA KOSA LANGU:

SIMULIZI YA KOSA LANGU:  AUTHOR : ADELA DALLY KAVISHE Joyce ni msichana aliyezaliwa katika familia ya watoto wawili akiwa ni mtoto wa kwanza katika familia ya Mzee Ndesanjo, maisha yao yalikuwa ni maisha ya furaha na amani walikuwa wakiishi Mkoa wa Dar es salaam maeneo ya Kimara Stop Over, lakini furaha hiyo ilipotea baada ya siku moja ambapo Mzee Ndesanjo alikuja nyumbani baada ya kutoka kazini na moja kwa moja akimtaka mama Joyce ajiandae kwani wangesafiri siku hiyo ambapo ilikuwa ni siku ya jumanne mida ya saa kumi na mbili jioni.Mzee Ndesanjo alikuwa na gari aina Eskudo alifika na kuita kwa sauti "Mama Joyce Mama Joyce" huko chumbani mama Joyce alimskia na kuitika "Bee Mume wangu,vipi mbona unaonge kwa sauti sana si ungeingia ndani kwanza" alisema mamaJocye huku akiwa anamuangalia mume wake kwa makini Baba Joyce alimsogelea huku akisema "hakuna muda wa kupoteza mimi ndani siingii nenda kajiandae tunasafari ya kwenda Morogoro kuna matatizo kwani rafiki yang