Skip to main content

WhatsApp kuzimwa katika simu hizi mwaka 2020


WhatsApp kuacha kufanya kazi katika mamilioni ya simu kuanzia mwaka 2020. Simu hizi ni matoleo ya nyuma ya simu zinazotumia Android, iOS na Windows Phone.

whatsapp app WhatsApp kuacha kufanya kazi
WhatsApp kuacha kufanya kazi: Je simu yako itaendelea kuwa na sifa?
Kampuni ya WhatsApp inayomilikiwa na Facebook imetoa taarifa ikisema inasikitika na uamuzi huu ila ni uamuzi wa kilazima kufanyika ili kuhakikisha wanaendelea kuwa na uwezo wa kuhakikisha watumiaji wake wanakuwa salama dhidi ya udukuzi ambao unaweza kufanywa kwenye matoleo ya nyuma ya programu endeshaji za simu.
Kwa watumiaji wa simu zenye sifa zifuatazo wajiandae kuona app ya WhatsApp ikisumbua kufanya kazi ifikapo Februari 1 2020, kama simu zao zinauwezo wa kupokea matoleo mapya ya programu endeshaji basi wanashauriwa kufanya hivyo.
Unatumia iPhone 5
Simu za iPhone 5 na 5S kutoka Apple zinaonekana kuwa ni baadhi maarufu ambazo zitaathirika kwa uamuzi huu. Bado zinatumika hasa kwa mataifa yanayoendelea. Tovuti ya DeviceAtlas ilisema kufikia mwaka huu simu za iPhone 5 na 5S zinawakilisha zaidi ya asilimia moja na nusu ya simu zinazitembelea tovuti mbalimbali mwaka huu.
  • Android – Kwa android ni kwa simu zinazotumia programu endeshaji ya 2.3.3 Gingerbread na kurudi nyuma. Kama unatumia simu yeyote ya Android (mfano kutoka Samsung, Huawei, Sony na Google) iliyotoka ndani ya kipindi cha miaka 10 iliyopita utakuwa salama.
  • iOS (iPhone) – Kwa simu za iPhone toleo lolote la programu endeshaji la iOS kuanzia la 8 kwenda nyuma hazitakuwa na sifa tena. iOS 8 ni programu endeshaji iliyotambulishwa mwaka 2014. Simu ya chini kabisa yenye sifa ya kupokea toleo la iOS la kisasa zaidi la iOS 8 ni simu ya iPhone 6. Hii inamaanisha kama unamiliki iPhone yeyote iliyotoka kabla ya iPhone 6 basi ujiandae app hiyo kutoweza kufanya kazi tena ifikapo Februari 1, 2020.
  • Windows Phones – Simu zote zinazotumia toleo la Windows 8.1 au lolote jipya ndio wataendelea kuwa na uwezo wa kutumia WhatsApp. Matoleo ya nyuma yake haitawezekana tena.
CREDIT https://teknolojia.co.tz/

Je una mtazamo gani kuhusu maamuzi haya kutoka WhatsApp? Je simu yako bado ina sifa?

Popular posts from this blog

DOWNLOAD; nyimbo mpya ya alikiba #JOHOTENA

Jinsi ya ku-track simu yako na kujua mahali ilipo

Upotevu wa simu yako ni moja ya jambo baya watu wanalipata.Unaweza kuibiwa simu yako iliyokuwa imehifadhi data nyingi binafsi. Kwa msaada jinsi ya kupata simu yako iliyopotea, Google na Apple kwa pamoja wana njia za kufuatilia hili kutafuta mfumo wa simu yako. Jinsi ya kutafuta iPhone iliyopotea Ufumbuzi wake upo kwenye Find My iPhone.Huduma hii ina uwezo wa kukuonyesha kifaa chako chochote cha iOS Kupata uwezo juu ya iPhone yako,fuata hatua hizi; 1.Nenda kwenye setting/mpangilio wa iPhone yako 2.Shuka chini utakuta iCloud 3.Katika chini ya orodha bonyeza "Find My iPhone" 4.Kwenye Find My Phone switch on position 5.Ukiwa hapo ni wazo zuri ku-turn on send last  location Baada ya kuwezesha Find My iPhone,unaweza kuifuatilia vizuri simu yako iliyopotea na kuibiwa Jinsi ya kupata Android phone Kwa android ni tofauti kidogo na Apple.Google wameweka app yao kwenye Play store  na unaweza ku-download 1.Search Play Store "Android Device Manager" 2.Inst

Tumia simu yako kama mounse ya komputa

New Trick Habari za wakati huu msomaji wa Blog yako pendwa ya  DODY BLOG ! Katika mfululizo wa makala za wiki hii, leo tutaangalia jinsi ya  KUTUMIA   simu yako hio ya  SmartPhone kama  Mouse  ya kompyuta. FAIDA >>>Hii inaweza kukusaidia pale ambapo hauna Mouse kwa ajili ya compyuta yako, au  TouchPad  ya Laptop yako haifanyi kazi! Yani  inasumbua! MAHITAJI >> Utahitajika kuinstall program na App ntakazokupa hapa chini! Unaweza kutumia Apps mbalimbali na step ni hizihizi.  Host file utaiinstall kwenye kompyuta yako na App utaiweka kwenye simu yako, halafu utaunga compyuta yako kwenye wireless ya simu yako au bluetooth!  (Lengo la kuunga ni kuweka mawasiliano kati ya simu na kompyuta). kwa hio unaweza kutumia  Bluetooth au Wireless!  Zote ni sawa ila hapa nitaelezea Wireless. HATUA KWA HATUA 1.   Download na install  Monect  kwenye simu yako  HAPA! Install Monect Portable 2. Kwenye PC yako download na install  Monect Host  kwa kuclik  HAPA