Haki miliki ya picha EXPENSIVE CHAT Je, kwa wewe mtumiaji wa simu ya mkononi na mitandao ya kijamii, umeshawahi kuwaza idadi ya herufi unazoandika katika mawasiliano kwa jamaa na marafiki zako au kutoa maoni au mawazo yako mitandaoni kuwa ipo siku huenda usimudu gharama yake?. Marc Kohlbrugge mjasiliamali wa mitandaoni ameanzisha ukurasa wa kupigia soga maarufu kama 'chat room', ambapo gharama yake kwa kuandika herufi moja ni kiasi cha dola 0.01 sawa na shilingi 23 za kitanzania kwa herufi moja. Marc amesema kuwa alianzisha ukurasa huo kama majaribio yake mtandaoni, lakini amesema mwitikio wake umekuwa mkubwa kwani hadi sasa ana watu 100 ambapo hadi sasa wamekwisha mlipa kiasi cha dola 335 sawa na shilingi 785,000 za kitanzania, kwa herufi 33,0500 ambazo wamekwisha zilipia. Suala la kupiga soga lilivyo zoeleka kwa sasa katika nchini za Afrika, Afrika Mashariki ikiwemo, sidhani kama kuna mtu anayeweza kumudu gharama,maana wapo watu ambao,tangu asubuhi hadi jioni kwa ucha