Skip to main content

Kizungumkuti chaibuka Chelsea, Conte kuondoka, Costa kubaki

Hali ya sintofahamu imezidi kuiandama klabu ya Chelsea, kumekuwa na matukio ambayo hayaeleweki toka msimu umeisha lakini kipigo cha juzi kutoka kwa Burnley kimezidi kuchafua hali ya hewa ndani ya Chelsea.
Image result for diego costa
Kama unakumbuka wiki chache baada ya dirisha la usajili ndani ya Chelsea kufunguliwa kuliibuka tetesi kwamba Antonio Conte amechukizwa na sera za usajili wa Chelsea hali iliyofikia kutaka kuondoka.
Moja ya malalamiko ya Conte ilikuwa ni kukosa userious katika suala la usajili jambo ambalo lilipelekea kukosa wachezaji awatakao akiwemo Romelu Lukaku na pia Conte akitaka kupewa nafasi kubwa zaidi katika maamuzi.
Maisha yakaendelea na Conte akasaini mkataba mpya lakini wiki hii suala hilo limejitokeza tena na taarifa zinasema hali sio shwari hata kidogo kati ya klabu ya Chelsea na Muitaliano huyo baada ya Conte kudai mabosi wanamuangusha.
Wachambuzi mbali mbali wa masuala ya soka barani Ulaya wameshaanza kutabiri kwamba huu ni msimu wa mwisho wa Conte huku wacheza kamari nao wakianza kubet kwamba Conte anaweza asimalize msimu huu wa ligi.
Wakati Conte akianza kutabiriwa kuondoka Chelsea kwingineko mshambuliaji aliyeko kwenye msuguano na kocha huyo Diego Costa ametakiwa kurejea klabuni hapo ili kujiunga na wenzake kwa ajili ya msimu wa ligi.
Itambulike kwamba Costa bado ni mchezaji wa Chelsea na bado ana mkataba nao hivyo klabu yake imeamua kumrejesha kikosini japo anatakiwa kwanza kuanza kufanya mazoezi na wachezaji wa akiba.
Diego Costa mwenyewe kuhusu kufanya mazoezi na timu ya wachezaji wa ziada amesema “sio sawa kwa sababu mimi sina tatizo na mimi sina kosa kama ni faina sawa tu acha wanikate”. Hadi sasa haijafahamika wazi kwamba Costa atabaki Chelsea au atapata timu mpya kama anavyotaka.

Comments

Popular posts from this blog

DOWNLOAD; nyimbo mpya ya alikiba #JOHOTENA

Jinsi ya ku-track simu yako na kujua mahali ilipo

Upotevu wa simu yako ni moja ya jambo baya watu wanalipata.Unaweza kuibiwa simu yako iliyokuwa imehifadhi data nyingi binafsi. Kwa msaada jinsi ya kupata simu yako iliyopotea, Google na Apple kwa pamoja wana njia za kufuatilia hili kutafuta mfumo wa simu yako. Jinsi ya kutafuta iPhone iliyopotea Ufumbuzi wake upo kwenye Find My iPhone.Huduma hii ina uwezo wa kukuonyesha kifaa chako chochote cha iOS Kupata uwezo juu ya iPhone yako,fuata hatua hizi; 1.Nenda kwenye setting/mpangilio wa iPhone yako 2.Shuka chini utakuta iCloud 3.Katika chini ya orodha bonyeza "Find My iPhone" 4.Kwenye Find My Phone switch on position 5.Ukiwa hapo ni wazo zuri ku-turn on send last  location Baada ya kuwezesha Find My iPhone,unaweza kuifuatilia vizuri simu yako iliyopotea na kuibiwa Jinsi ya kupata Android phone Kwa android ni tofauti kidogo na Apple.Google wameweka app yao kwenye Play store  na unaweza ku-download 1.Search Play Store "Android Device Manager" 2.Inst

Tumia simu yako kama mounse ya komputa

New Trick Habari za wakati huu msomaji wa Blog yako pendwa ya  DODY BLOG ! Katika mfululizo wa makala za wiki hii, leo tutaangalia jinsi ya  KUTUMIA   simu yako hio ya  SmartPhone kama  Mouse  ya kompyuta. FAIDA >>>Hii inaweza kukusaidia pale ambapo hauna Mouse kwa ajili ya compyuta yako, au  TouchPad  ya Laptop yako haifanyi kazi! Yani  inasumbua! MAHITAJI >> Utahitajika kuinstall program na App ntakazokupa hapa chini! Unaweza kutumia Apps mbalimbali na step ni hizihizi.  Host file utaiinstall kwenye kompyuta yako na App utaiweka kwenye simu yako, halafu utaunga compyuta yako kwenye wireless ya simu yako au bluetooth!  (Lengo la kuunga ni kuweka mawasiliano kati ya simu na kompyuta). kwa hio unaweza kutumia  Bluetooth au Wireless!  Zote ni sawa ila hapa nitaelezea Wireless. HATUA KWA HATUA 1.   Download na install  Monect  kwenye simu yako  HAPA! Install Monect Portable 2. Kwenye PC yako download na install  Monect Host  kwa kuclik  HAPA