Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2019

yajue mambo 5 ya mafanikio kwako

Kila binadamu ameumbwa na kiu ya kufanikiwa katika kila kitu anachofanya. Mafanikio ndio kilele cha mlima mkubwa wa maisha ambao umejengwa kwa misingi na ngazi za mihangaiko na mitihani ambayo unapaswa kuivuka ili upumzike kwenye kilele hicho. Kwa bahati mbaya, unaposema ‘mafanikio’ wengi hufikiria kuhusu ‘utajiri’. Lakini ukweli ni kuwa kuna tofauti kati ya kuwa tajiri na kufanikiwa kiuchumi. Unaweza kuwa tajiri lakini ukawa bado hujafanikiwa. Kwa kuwa watu wanawaza utajiri kuwa ndio kigezo cha mafanikio hujikuta wakijiingiza kwenye vitendo vya ajabu kwa lengo la kujizolea mali lakini mwisho huwa wanagundua kuwa hawajafanikiwa japo jamii inahisi wamefanikiwa. Njia rahisi za Kumgeuza Rafiki kuwa ‘Mpenzi Wako’ wa Dhati Nanachoamini mimi, kufanikiwa kweli ni kutimiza malengo yako kwa ufanisi na kwa wakati, lakini mafanikio hayo yakupe amani moyoni mwako (peace of mind). Vinginevyo, utafanikiwa kwa mrundikano wa fedha huku ukitengeneza tatizo kubwa zaidi la msongo wa mawazo na u

zinduka,, hizi ni njia za mafanikio

MTU anafanikiwa kikweli kwa kupata njia bora kabisa ya maisha ambayo inatokana na kufuata viwango vya Mungu na kuishi kupatana na kusudi la Mungu kwa wanadamu. Biblia inasema kwamba mtu anayeishi maisha ya aina hiyo “atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao hutoa matunda yake katika majira yake na ambao majani yake hayanyauki, na  kila jambo analofanya litafanikiwa.” — Zaburi 1:3 . Naam, ingawa sisi si wakamilifu na tunafanya makosa, tunaweza kufanikiwa maishani! Je, hilo linakuvutia? Ikiwa ndivyo, basi kanuni sita zinazofuata za Biblia zinaweza kukusaidia ufikie lengo hilo na hivyo kuthibitisha waziwazi kwamba kwa kweli mafundisho ya Biblia ni hekima inayotoka kwa Mungu.— Yakobo 3:17 . 1 Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Pesa “Kupenda pesa ni chanzo cha mambo mabaya ya namna zote, na kwa kujitahidi kufikia upendo huo wengine . . . wamejichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.” ( 1 Timotheo 6:10 ) Ona kwamba tatizo si pesa, kwa kuwa sisi sote tunahitaji pesa