Ticker

6/recent/ticker-posts

TETESI ZA USAJILI KATIKA MAGAZETI YA UINGEREZA LUIZ TO MAN U

Daily Express. Kocha wa Manchester United Jose Mourinho anatajwa kuwa mbionj kujaribu kumshawishi David Luiz ajiunge naye ifikapo mwezi wa kwanza baada ya beki huyo kutajwa kutokuwa na mahusiano mazuri na kocha wa Chelsea.
Daily Mirror. Klabu ya Liverpool sasa italazimika kutoa kiasi cha £70m kwa ajili ya kumnunua mliniz wa Southampton Virgil Van Djik ambaye wamekuwa wakimtaka kwa muda mrefu na sasa kocha wa Southampton amesema wako tayari kumuachia kama wakipata kiasi hicho.
Daily Star. Steve Kaplan ambaye ni moja kati ya wamiliki wa klabu ya Swansea amepiga kura ya kutokuwa na imani na kocha wa Swansea Paul Clement na sasa kocha huyo anakuwa amekalia kuti kavu ndani ya klabu hiyo.
The Sun. Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Arsenal na pia Manchester City Emmanuel Adebayor ameishutumu familia yake kwamba ilimfanya atamani kujiua zaidi ya mara tatu kutokana na matatizo yaliyosababishwa na familia hiyo.
Daily Mail. Klabu ya soka ya Manchester United imezipiga chini tetesi za Jose Mourinho kuhamia PSG na kusisitiza kwamba tetesi hizo sio za kweli kwani kocha huyo bado atakaa Old Traford kwa muda mrefu zaidi.

Post a Comment

0 Comments