Skip to main content

Tetesi za usajili ulaya jumamosi tareh 30/12/2017


 https://images.enca.com/encadrupal/styles/600_383/s3/WEB_PHOTO_Cristiano+Ronaldo_2.jpg
Cristiano Ronaldo
Cristiano Ronaldo ameitaka klabu ya Real Madrid kuweka bei yao ya kumuuza isiopungua £89m). Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 kutoka Ureno yuko tayari kuondoka Uhispania.(Daily Record)
Mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard, 26, hajakaataa kuongeza kandarasi na mabingwa hao watetezi wa Uingereza licha ya madai kutoka kwa babake kwamba anataka kuhamia Real Madrid.(Independent)
 
Related image
  Eden Hazard
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger anajiandaa kumnunua winga wa Ivory Coast na Crystal Palace Zaha ili kuchukua mahala pake mshambulijai wa Chile Alexis Sanchez, 29. (Daily Star)
Wachezaji kadhaa wa Arsenal walidaiwa kumshutumu mshambuliaji Alexi Sanchez kwa kuwa na tabia mbaya baada ya mechi dhidi ya Burnley mwezi Novemba. (Guardian)
  Related image
Winfred Zaha
Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp anasema kuwa usajili wa kitita cha £75m wa beki wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 26 Virgil van Dijk kutoka Southampton haumanishi kwamba klabu hiyo sasa itamuuza Philippe Coutinho, lakini hakusema kuwa mchezaji huyo hataondoka Liverpool. (Daily Mail)
Mkufunzi wa Chelsea Antonio Conte anajiandaa kumnunua kiungo wa kati wa Everton na Uingereza Ross Barkley, 24. (Telegraph)
Image result for Ross Barkley 
Ross Barkley
Manchester United inamchunguza kiungo wa kati wa Napoli na Itali Jorginho, 26, ili kuchukua mahala pake Michael Carrick. (Manchester Evening News)
West Ham itawasilisha ombi la kutaka kumsajili kiungo wa kati wa Uingereza Jonjo Shelvey, 25, huku David Moyes akijaribu kuimarisha safu yake ya kati.. (Daily Mirror)
Related image
Otamendi
Manchester City itampatia beki Nicolas Otamendi kandarasi mpya.Mchezaji huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 29 alitia kandarasi ya miaka 5 mwaka 2015(ESPN)
Nahodha wa West Brom Jonny Evans analengwa na klabu ya ManCity.
Mkufunzi wa klabu hiyo Alan Pardew alikiri kwamba klabu hiyo ingependelea kumuuza beki wa Ireland kaskazini Evans ili kukusanya fedha za kununua mshambuliaji (Mirror)
Related image
Henrikh Mkhitaryan, 28.
Inter Milan inajiandaa kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United na Armenia Henrikh Mkhitaryan, 28. (Sky Sports)
Mshambuliaji wa Liverpool Daniel Sturridge anapendelea uhamisho wa Southampton lakini anahofia United itazuia uhamisho wowote chini ya £25m. (Daily Mirror)
Hatahivyo Southampton inakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa Stoke ambayo inajiandaa kuongeza kiungo wa kati mwengine katika kikosi chake. (Mail)

 Related image
Daniel Sturridge
Liverpool itamsajili kiungo wa kati wa Schalke's na Ujerumani Leon Goretzka katika uhamisho wa bure msimu ujao(Sun via Bild)
Juventus iko tayari kuanzisha makubaliano ya kuweka kandarasi na kiungo wa kati wa Liverpool na Ujerumani Emre Can, 23. (Corriere dello Sport - in Italian)
Mkurugenzi wa Everton Steve Walsh amesafiri hadi mjini Istanbul Uturuki ili kukamilisha uhamisho wa mshambuliaji wa Besiktas Cenk Tosun, 26, kufuatia waiwasi kutoka kwa vilabu vyengine vya Uturuki vinavyomuwinda (Times - subscription required)

Comments

Popular posts from this blog

DOWNLOAD; nyimbo mpya ya alikiba #JOHOTENA

Jinsi ya ku-track simu yako na kujua mahali ilipo

Upotevu wa simu yako ni moja ya jambo baya watu wanalipata.Unaweza kuibiwa simu yako iliyokuwa imehifadhi data nyingi binafsi. Kwa msaada jinsi ya kupata simu yako iliyopotea, Google na Apple kwa pamoja wana njia za kufuatilia hili kutafuta mfumo wa simu yako. Jinsi ya kutafuta iPhone iliyopotea Ufumbuzi wake upo kwenye Find My iPhone.Huduma hii ina uwezo wa kukuonyesha kifaa chako chochote cha iOS Kupata uwezo juu ya iPhone yako,fuata hatua hizi; 1.Nenda kwenye setting/mpangilio wa iPhone yako 2.Shuka chini utakuta iCloud 3.Katika chini ya orodha bonyeza "Find My iPhone" 4.Kwenye Find My Phone switch on position 5.Ukiwa hapo ni wazo zuri ku-turn on send last  location Baada ya kuwezesha Find My iPhone,unaweza kuifuatilia vizuri simu yako iliyopotea na kuibiwa Jinsi ya kupata Android phone Kwa android ni tofauti kidogo na Apple.Google wameweka app yao kwenye Play store  na unaweza ku-download 1.Search Play Store "Android Device Manager" 2.Inst

Tumia simu yako kama mounse ya komputa

New Trick Habari za wakati huu msomaji wa Blog yako pendwa ya  DODY BLOG ! Katika mfululizo wa makala za wiki hii, leo tutaangalia jinsi ya  KUTUMIA   simu yako hio ya  SmartPhone kama  Mouse  ya kompyuta. FAIDA >>>Hii inaweza kukusaidia pale ambapo hauna Mouse kwa ajili ya compyuta yako, au  TouchPad  ya Laptop yako haifanyi kazi! Yani  inasumbua! MAHITAJI >> Utahitajika kuinstall program na App ntakazokupa hapa chini! Unaweza kutumia Apps mbalimbali na step ni hizihizi.  Host file utaiinstall kwenye kompyuta yako na App utaiweka kwenye simu yako, halafu utaunga compyuta yako kwenye wireless ya simu yako au bluetooth!  (Lengo la kuunga ni kuweka mawasiliano kati ya simu na kompyuta). kwa hio unaweza kutumia  Bluetooth au Wireless!  Zote ni sawa ila hapa nitaelezea Wireless. HATUA KWA HATUA 1.   Download na install  Monect  kwenye simu yako  HAPA! Install Monect Portable 2. Kwenye PC yako download na install  Monect Host  kwa kuclik  HAPA