Skip to main content

Man Pacquiao akutana na mbabe damu zatapakaa ulingoni

Hatimaye bondia wa Australia, Jeff Horn ambaye alikuwa mwalimu shuleni ameishangaza dunia kwa kumpiga bondia Mfilipino mwenye cheo cha Useneta, Manny Pacquiao na kuendeleza rekodi ya kutoshindwa pambano.
Horn (17-0-1) ambaye alikuwa hapewi nafasi na wadau wa masumbwi duniani kwenye pambano hilo lililomalizika dakika chache zilizopita, amemnyang’anya Pacquiao mkanda wa ubingwa wa ngumi wa dunia wa WBO wa uzito wa welterweight baada ya raundi 12 nzito za pambano hilo lililofanyika nchini Australia kwenye uwanja wa mpira na kuhudhuriwa na zaidi ya watazamaji 55,000.
Majaji wa pambano hilo wamempa ushindi Horn dhidi ya Pacquiao kwa point 117-111 & 115-113 (X2), huku pambano hilo likitawaliwa na damu kutoka kwenye majeraha yawapiganaji hao. Ilikuwa ni vita kama ilivyoahidiwa na wote.
Alipoulizwa kama anahitaji pambano la marudiano, Horn ambaye alionekana kucheza ‘rafu’ katika raundi nyingi alijibu, “niko tayari, leteni tena [pambano la marudiano].”
Kwa ushindi huo, Horn ambaye alikuwa anatajwa na wadau kama bondia asiyejulikana, ameingia rasmi kwenye mkondo mkuu wa masumbwi duniani na sasa anaweza kutajwa kuwa tishio kwa mabondia wengi wenye majina Marekani, na huenda akaingia kwenye rekodi ya wanaoweza kupambana na Floyd Mayweather.
Kwa Pacquiao, kupoteza pambano hili ni pigo kwa ndoto yake ya kutaka pambano la marudiaono dhidi ya Mayweather ambaye amerejea akijiandaa na pambano kati yake na bingwa wa UFC, Conor McGregor.

Comments

Popular posts from this blog

DOWNLOAD; nyimbo mpya ya alikiba #JOHOTENA

Jinsi ya ku-track simu yako na kujua mahali ilipo

Upotevu wa simu yako ni moja ya jambo baya watu wanalipata.Unaweza kuibiwa simu yako iliyokuwa imehifadhi data nyingi binafsi. Kwa msaada jinsi ya kupata simu yako iliyopotea, Google na Apple kwa pamoja wana njia za kufuatilia hili kutafuta mfumo wa simu yako. Jinsi ya kutafuta iPhone iliyopotea Ufumbuzi wake upo kwenye Find My iPhone.Huduma hii ina uwezo wa kukuonyesha kifaa chako chochote cha iOS Kupata uwezo juu ya iPhone yako,fuata hatua hizi; 1.Nenda kwenye setting/mpangilio wa iPhone yako 2.Shuka chini utakuta iCloud 3.Katika chini ya orodha bonyeza "Find My iPhone" 4.Kwenye Find My Phone switch on position 5.Ukiwa hapo ni wazo zuri ku-turn on send last  location Baada ya kuwezesha Find My iPhone,unaweza kuifuatilia vizuri simu yako iliyopotea na kuibiwa Jinsi ya kupata Android phone Kwa android ni tofauti kidogo na Apple.Google wameweka app yao kwenye Play store  na unaweza ku-download 1.Search Play Store "Android Device Manager" 2.Inst

Tumia simu yako kama mounse ya komputa

New Trick Habari za wakati huu msomaji wa Blog yako pendwa ya  DODY BLOG ! Katika mfululizo wa makala za wiki hii, leo tutaangalia jinsi ya  KUTUMIA   simu yako hio ya  SmartPhone kama  Mouse  ya kompyuta. FAIDA >>>Hii inaweza kukusaidia pale ambapo hauna Mouse kwa ajili ya compyuta yako, au  TouchPad  ya Laptop yako haifanyi kazi! Yani  inasumbua! MAHITAJI >> Utahitajika kuinstall program na App ntakazokupa hapa chini! Unaweza kutumia Apps mbalimbali na step ni hizihizi.  Host file utaiinstall kwenye kompyuta yako na App utaiweka kwenye simu yako, halafu utaunga compyuta yako kwenye wireless ya simu yako au bluetooth!  (Lengo la kuunga ni kuweka mawasiliano kati ya simu na kompyuta). kwa hio unaweza kutumia  Bluetooth au Wireless!  Zote ni sawa ila hapa nitaelezea Wireless. HATUA KWA HATUA 1.   Download na install  Monect  kwenye simu yako  HAPA! Install Monect Portable 2. Kwenye PC yako download na install  Monect Host  kwa kuclik  HAPA